Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.
Mataifa yote yakusanyike, watu wote wakutane pamoja. Nani kati ya miungu yao anayeweza kutangaza yatakayotukia? Nani anayeweza kutuonyesha yanayotukia sasa? Wawalete washuhuda wao, kuhakikisha kwamba walifanya hivyo. Uwaache wasikilize na kusema: Ilikuwa kweli.