Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 41:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 41:20
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nani kati ya viumbe hivyo, asiyejua kwamba Yawe ametenda yale?


Uwaonyeshe watu kuwa wewe ndiwe uliyetenda hayo. Wewe, ee Yawe, ndiwe uliyefanya hivyo.


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Ujuzi huu nao unatoka kwa Yawe wa majeshi. Mipango yake ni ya ajabu, hekima yake ni kamilifu kabisa.


Waliopotoka katika roho watapata maarifa na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.


Kisha utukufu wa Yawe utafunuliwa, na watu wote pamoja watauona. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.


Mimi ni Yawe, Mutakatifu wenu; Mimi ndiye Muumba wa Israeli, Mufalme wenu.


watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, kusudi wazitangaze sifa zangu!


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Ninayajua matendo yao na mawazo yao. Ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na wa luga zote, wakusanyike pamoja na kuuona utukufu wangu.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hakika ulozi hauwezi kuwapinga watu wa Yakobo, wala uchawi juu ya watu wa Israeli. Sasa juu ya Israeli, watu watasema: Muangalie maajabu Mungu aliyotenda!


atakapokuja apate kutukuzwa na watu wake na kushangiliwa na wale wote wanaoamini. Ninyi vilevile mutakuwa pamoja nao kwa maana mumeamini habari tuliyowatangazia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ