Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 41:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Nitawafanya mukuwe kama chombo cha kupepeta, chenye meno mapya na makali. Mutaipepeta milima na kuipondaponda; mutavisagasaga vilima kama maganda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 41:15
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walitafuta musaada, lakini hakukukuwa wa kuwasaidia; walimulilia Yawe, lakini hakuwajibu.


Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.


Ewe Israeli, watu wangu, enyi muliotwangwa na kupepetwa kama ngano. Sasa nimewaambia ninyi mambo niliyoyasikia kwa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli.


Kunde haipepetwi kwa chombo kikali wala mbegu za vikolezo kwa gari! Lakini kunde zinapepetwa kwa fimbo na mbegu za vikolezo kwa kijiti.


Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.


Nitaharibu milima na vilima, na majani yote nitayakausha. Mito ya maji nitaigeuza kuwa inchi kavu, na visima vya maji nitavikausha.


Ingeteketea kama moto unavyochoma kichaka, kama vile moto unavyochemusha maji. Ukuje upate kuwajulisha waadui zako jina lako nayo mataifa yatetemeke mbele yako!


Yawe anasema hivi: Wewe Babeli ni nyundo na silaha yangu ya vita; ninakutumia kwa kuyavunjavunja mataifa, ninakutumia kwa kuangamiza falme.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Babeli ni kama uwanja wa kupepetea ngano wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Nitaifanya inchi kuwa jangwa na tupu. Nitawaua mashujaa wake wenye kiburi. Milima ya inchi ya Israeli itakuwa jangwa na hakuna mutu atakayepita huko.


Mara moja chuma, udongo wa mufinyanzi, shaba, feza na zahabu, vyote vikavunjika vipandevipande na vikakuwa kama maganda kwenye nafasi ya kupepetea ngano wakati wa jua. Upepo ukavipeperushia mbali wala hakukubakia hata kipande kimoja. Lakini lile jiwe lililoivunja ile sanamu likageuka kuwa mulima mukubwa na kuijaza dunia yote.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Kwa kasirani ulipita juu ya inchi, uliyakanyaga mataifa kwa hasira yako.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


lakini tena inchi ya milima itakuwa yenu. Ingawa sasa ni pori, mutaifyeka na kuirizi yote toka upande huu mpaka upande mwingine. Mutawaondoa Wakanana, hata kama wana magari ya chuma na ni wenye nguvu.”


Yawe akamwambia: “Nitakuwa pamoja nawe; nawe utawaangamiza Wamidiani sawa vile wangekuwa mutu mumoja.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ