Isaya 41:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.
Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
Mataifa yote yakusanyike, watu wote wakutane pamoja. Nani kati ya miungu yao anayeweza kutangaza yatakayotukia? Nani anayeweza kutuonyesha yanayotukia sasa? Wawalete washuhuda wao, kuhakikisha kwamba walifanya hivyo. Uwaache wasikilize na kusema: Ilikuwa kweli.
Musogee karibu nami musikie jambo hili: Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri, tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwa pale. Sasa, Bwana wetu Yawe amenituma, na kunipa nguvu ya Roho wake.
Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.
Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.