Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 40:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 40:9
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Abiya akasimama juu ya mulima Zemaraimu, unaokuwa kati ya milima ya Efuraimu akamwambia Yeroboamu na Waisraeli: “Unisikilize, ewe Yeroboamu na Waisraeli wote!


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.


Mimi ni yule wa kwanza. Nilitangaza kwa Sayuni, nikapeleka Yerusalema mujumbe wa habari njema.


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Kwa hiyo watu wangu watajua mimi ni nani. Siku hiyo watajua kwamba ni mimi ninayesema: “Niko!”


Munafunga kula lakini munagombana na kupigana mangumi vikali. Mukifunga namna hiyo, maombi yenu hayatafika kwangu juu.


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Enyi watu wa Yerusalema, mupande kwa milima ya Lebanoni mupige kelele, munyanyue sauti zenu huko kwenye uwanja wa Basani; mulalamike kutoka milima ya Abarimu, maana wapenzi wenu wote wameangamizwa.


Maana, mimi ninajua mupango ninaokuwa nao juu yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nayo mipango yangu ni ya kuwatendea mema wala si mabaya, kusudi mupate kuwa na tumaini katika siku zinazokuja.


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


Basi Petro akasimama pamoja na wale mitume wengine kumi na mumoja na kuanza kusema kwa sauti kubwa mbele ya watu: “Ninyi Wayuda, nanyi wote munaokaa Yerusalema, musikilize vizuri, mutege sikio kwa maneno nitakayowaambia.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Na sasa Ee Bwana, angalia vitisho vyao. Basi utuwezeshe sisi watumishi wako tupate kutangaza neno lako kwa uhodari kabisa.


Basi ninauliza: hawakusikia habari hii? Ndiyo, wameisikia! Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Sauti yao imesikilika katika dunia yote, maneno yao yamefika pande zote za dunia.”


Muniombee vilevile, kusudi Mungu anijalie maneno ya kusema. Kwa hiyo nitaweza kuwajulisha watu kwa uhodari siri ya Habari Njema.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Hata mukiteswa kwa ajili ya haki, ninyi ni wenye heri. Musiwaogope watu, wala musihangaike.


Yotamu alipopata habari hiyo, alikwenda kusimama juu ya mulima Gerizimu, akasema kwa sauti kubwa: “Munisikilize, enyi watu wa Sekemu kama munataka Mungu awasikilize.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ