Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 40:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 40:31
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.


Anajaza maisha yangu na raha, hata ninabaki kijana mwenye nguvu kama tai.


Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma.


Nilipokulilia, wewe ulinijibu; umeniongezea nguvu yangu.


Hao wanajikwaa na kuanguka; lakini sisi tunasimama na kuimarika.


Ukamilifu na usawa vinanikinga, maana ninakutumainia wewe.


Usimwache anayekutumainia kupata haya; lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.


Uniongoze katika ukweli wako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu, mwokozi wangu; ninakutegemea wewe kila siku.


Umutumainie Yawe na kushika njia yake, naye atakuinua uirizi inchi, na kuwaona waovu wakiongolewa.


Wanapopita katika bonde lenye kukauka la Baka, wanalifanya kuwa chemichemi, nazo mvua za kwanza zinalijaza maji.


Wanaendelea wakipata nguvu zaidi na zaidi: watamwona Mungu wa miungu huko Sayuni.


Watu wa haki wanastawi kama mingazi; wanakomaa kama mierezi ya Lebanoni!


‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.


njia ya tai katika anga, njia ya nyoka juu ya jiwe, njia ya mashua ndani ya bahari, na njia ya mwanaume kwa mwanamuke.


Ni nani huyu anayekuja kutoka katika jangwa, akimwegemea mupenzi wake? Mimi nilikuamusha chini ya muti wa mutofaa, pale ambapo mama yako aliona uchungu, pale ambapo mama yako alikuzaa.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Mwangamizaji wa Moabu na miji yake anashambulia, vijana wake wazuri wamechinjwa. –Ni ujumbe wa Mufalme, jina lake Yawe wa majeshi.–


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.


Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu.


Kwa wema wake, Mungu ametupatia utumishi huu, na kwa sababu hii sisi hatukati tumaini.


Kwa sababu hii hatukati tumaini hata kidogo. Ijapokuwa hali yetu ya kimwili inaharibika, hali yetu ya kiroho inafanywa upya siku kwa siku.


Tusichoke kutenda mema; kwa maana siku zitakapotimia tutavuna kama tusiporegea.


Alikuwa kama tai anayelinda chicha yake, anayeruka karibu ya vitoto vyake, akitandaza mabawa yake kwa kuwashikilia, na kuwabeba juu ya mabawa yake.


Miji yako itakuwa ya chuma na shaba. Usalama wako utadumu maisha yako yote!”


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa.


Kwa hiyo mumukumbuke yule aliyevumilia kutendewa na wenye zambi kwa chuki kubwa, kusudi musipate kuchoka wala kuregea.


Lakini bado nina nguvu kama nilivyokuwa wakati ule Musa aliponituma. Hata sasa nina nguvu za kuweza kupigana vita au kufanya kazi nyingine yoyote.


Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Wewe ni muvumilivu; umeteswa kwa ajili ya jina langu, lakini haukuregea.


Kiumbe cha kwanza kilifanana na simba, kiumbe cha pili kilifanana na mwana-ngombe na kiumbe cha tatu kilifanana na mutu na kiumbe cha ine kilifanana na tai anayeruka.


Hapo Samusoni akamwomba Yawe: “Bwana wangu Yawe, ninakuomba unikumbuke. Unitie nguvu, mara hii moja tu, ee Mungu, kusudi niwalipize kisasi mara moja hii tu Wafilistini ambao waliyaongoa macho yangu mawili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ