Wewe, ee Yawe, ndiwe Mungu wangu; nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana umetenda mambo ya ajabu; unaitimiza kwa uaminifu na kweli mipango uliyoipanga tangu zamani.
Yawe anasema hivi: Ewe Israeli, watu wa Yakobo, kumbuka kwamba wewe ni mutumishi wangu. Nilikuumba kusudi ukuwe mutumishi wangu, nami sitakusahau hata kidogo.
Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.
Daudi akajisemesha ndani ya moyo: “Siku moja, Saulo ataniangamiza. Jambo zuri kwangu ni kukimbilia katika inchi ya Wafilistini. Saulo atakata tamaa kunitafuta ndani ya mipaka ya inchi ya Israeli, nami nitakuwa salama kutoka katika mikono yake.”