Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 40:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Dunia iliumbwa na yule anayeikaa juu ya mbingu; kutoka huko wakaaji wa dunia ni kama mapanzi! Yeye ametandika mbingu kama pazia, na kuzikunjua kama hema la kuishi ndani yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 40:22
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akasema: “Anga likuwe katikati ya maji, litenge maji sehemu mbili.”


Mawingu mazito yamemuzunguka asipate kuona; anatembea inje ya anga la dunia!”


Mungu anatandaza kaskazini juu ya pahali patupu, na anatundika dunia pahali pasipo kuwa kitu.


Nani anayejua jinsi mawingu yanavyotanda, au jinsi radi inavyonguruma kwake katika anga?


Unaweza kuzitandaza mbingu kama yeye hata zikuwe ngumu kama kioo cha shaba?


Yeye peke yake alitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.


Umejifunika mwangaza kama kanzu, umekunjua mbingu kama hema;


Alipanda juu ya kerubi na kuruka, akaruka juu ya mabawa ya upepo.


Si kwa musemo au kwa maneno; wala hakuna sauti inayosikilika;


Yule anayetawala juu mbinguni anawachekelea na kuwazarau.


Yawe ameikaa juu ya mafuriko ya maji; Yawe ni mufalme anayetawala milele.


Enyi falme za dunia, mumwimbie Mungu, mumwimbie Bwana wetu nyimbo za sifa,


Nilikuwa niko wakati alipoweka mbingu, wakati alipofanya muviringo juu ya bahari;


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


“Ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.


Kwake mataifa ni kama tone la maji katika mbeketi, ni kama mavumbi juu ya kilo. Kwake visanga ni vyepesi kama mavumbi laini.


Mataifa yote si kitu mbele yake; kwake ni vitu vya ovyo na bure kabisa.


Yeye hataregea wala kuchoka, mpaka atakapoimarisha sheria yangu katika dunia. Watu wa mbali wanangojea mafundisho yake.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu na kuzitandika kama hema, aliyeifanya dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, anayewapa watu wanaokaa ndani yake uzima, na kuwajalia uzima wote wanaoishi ndani yake:


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Wewe umenisahau mimi Yawe Muumba wako, niliyezitandaza mbingu, na kuiweka misingi ya dunia! Kwa sababu ya kasirani ya yule anayekutesa, unaendelea kuogopa siku zote kwamba yuko tayari kukuangamiza! Lakini hasira yake itafikia wapi?


Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?


Yawe aliiumba dunia kwa nguvu zake; kwa hekima yake alisimamisha ulimwengu imara, kwa akili yake alizitandika mbingu juu.


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Tuliona majitu huko, wazao wa Anaki. Sisi tulijiona kuwa kama mapanzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona sisi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ