Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 4:2
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wakusifu, ee Mungu, watu wote wakusifu!


Inchi itoe mazao kwa wingi, vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni, na watu wa miji wastawi kama majani.


Utamushonea ndugu yako Haruni nguo takatifu kusudi apate kuonekana mwenye utukufu na muzuri.


Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Itakuja siku wazao wa Yakobo watatoa mizizi; watu wa Israeli watachanua na kuchipuka, na kuijaza dunia yote kwa matunda.


Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.


Enyi mbingu, munyeshe umande kutoka kule juu, mawingu yatiririshe ushindi; dunia ifuguke, ichipushe wokovu, na kuotesha haki vilevile! Mimi, Yawe nimefanya hayo.


Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Hivyo, kama vile udongo unavyootesha mimea, na shamba linavyochipukiza mbegu zilizopandwa humo, Yawe atasababisha haki na sifa kuonekana mbele ya mataifa yote.


Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Katika siku hizo, katika wakati huo, nitaotesha chipukizi wa haki wa uzao wa Daudi. Chipukizi huyo ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Kwa hiyo hakutakuwa mutu hata mumoja kati ya watu wa Yuda waliobaki na kwenda kukaa katika inchi ya Misri ambaye ataponyoka au kuishi au kurudi katika inchi ya Yuda ambayo wanatamani kurudi na kuishi humo. Hawatarudi, isipokuwa tu wakimbizi wachache.


Ni wachache tu ndio watakaoponyoka katika vita na kurudi kutoka inchi ya Misri na kwenda katika inchi ya Yuda. Halafu Wayuda wote waliobaki kati ya wale waliokwenda kukaa Misri watatambua ni neno la nani lenye nguvu: langu au lao!


Nitawapa mashamba yenye mboleo kusudi wasiangamizwe tena na njaa katika inchi ile, wala kuzarauliwa tena na mataifa mengine.


Lakini juu ya milima ya Waisraeli, miti itatoa matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Waisraeli, maana wao wanakaribia kurudi katika inchi yao.


Ikiwa kuna watu walioponyoka, watakimbilia kwenye milima kama njiwa waliotishwa katika bonde. Kila mumoja wao ataomboleza kwa ajili ya zambi zake.


Lakini wale waliobaki watakaa kwa mulima Sayuni nao utakuwa mulima mutakatifu. Wazao wa Yakobo watanyanganya inchi yao toka kwa wale waliokuwa wameinyanganya.


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa! Vijana wanaume na wanawake watastawi kwa wingi wa ngano na divai mupya.


Kisha Yawe wa majeshi akasema hivi: Hao watakuwa watu wangu. Watakuwa urizi wangu wa kipekee siku ile nitakaposimama kufanya jambo ninalokusudia. Sitawazuru kama vile baba asivyomuzuru mwana wake anayemutumikia.


Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.


Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ