na Yoyakini mufalme wa Yuda alijitoa kwa mufalme wa Babeli, yeye mwenyewe pamoja na mama yake, watumishi wake, wakubwa na majemadari wake. Mufalme wa Babeli aliwapeleka kama wafungwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake.
Alimupeleka Yoyakini mpaka Babeli pamoja na mama ya mufalme, wake za mufalme, wakubwa wa waaskari wake, na wakubwa wa inchi wote. Hao aliwatoa Yerusalema. Akawapeleka katika uhamisho kule Babeli.
Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.
Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema.
Watu waliookolewa kwenye vita aliwapeleka katika uhamisho Babeli. Kule wakakuwa watumwa wake na wa wazao wake mpaka ufalme wa Persia ulipoinuka kwa nguvu.