Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 39:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Siku zinakuja ambapo vyote vinavyokuwa katika nyumba yako na vitu vyote babu zako walivyokusanya mpaka leo, vitapelekwa Babeli. Hakuna kitu chochote kitakachobaki. –Ni Yawe anayesema hivyo.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 39:6
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.


Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema.


Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.


Zaidi ya hiyo, utajiri wote wa muji, mapato yake yote, vitu vyake vyote vya bei kali pamoja na akiba zote za wafalme wa Yuda, nitavitoa katika mikono ya waadui, ambao watavinyanganya na kuvipeleka Babeli.


Watakuvua nguo zako na kukunyanganya vitu vyako vizuri vya bei kali.


Bwana akamwacha Yoyakimu atiwe katika mikono ya mufalme Nebukadneza pamoja na sehemu ya vyombo vya nyumba ya Mungu. Basi mufalme Nebukadneza akakamata wafungwa na vyombo akavipeleka katika inchi ya Babeli, akaviweka katika hazina ya nyumba ya miungu yake.


Mufalme Nebukadneza akamwamuru Aspenazi, mukubwa wa watumishi wake, amuchagulie kati ya vijana wa Waisraeli wa jamaa ya kifalme na ya watu wenye heshima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ