Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 38:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kwenda umwambie Hezekia kwamba: Mungu wa baba yako Daudi, anasema hivi: Nimesikia ombi lako na nimeyaona machozi yako. Basi, ninakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 38:5
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, Yawe alimupatia Abiyamu mwana atakayetawala nyuma yake, kuwa taa ya kuangaza Yerusalema na kuuweka imara Yerusalema.


Kwa hiyo, sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba vilevile utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu mumoja wa uzao wako kwa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako watakuwa waangalifu juu ya mwenendo wao mbele yangu kama wewe ulivyofanya mbele yangu.’


Katika mwaka wa kumi na ine wa utawala wa mufalme Hezekia, mufalme Saniharibu wa Asuria aliishambulia miji yote yenye kuta ya Yuda na kuiteka.


Alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala. Akatawala miaka makumi mbili na tisa akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Abi binti ya Zakaria.


Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe kwa Hezekia, akisema: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: Nimesikia ombi lako kwangu juu ya Saniharibu mufalme wa Asuria.


Katika mwaka wa ine wa utawala wake, mufalme Yosia, akiwa bado kijana, alianza kumwabudu Mungu wa Daudi, babu yake. Kisha alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili alianza kusafisha inchi ya Yuda na Yerusalema kwa kuharibu pahali pa kutambikia miungu mingine, sanamu za Ashera, na sanamu zingine za kuchonga na za kuyeyusha.


Siku za kuishi za mwanadamu zimepimwa. Ee Mungu, umepanga hesabu ya miezi yake; hawezi kupita mupaka uliomwekea.


Kifo cha waaminifu wa Yawe si jambo dogo mbele yake.


Anawaponyesha waliovunjika moyo; na kuwatunza vidonda vyao.


Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao, uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.


Muondoke karibu nami, enyi wote watenda maovu! Maana Yawe amesikia kilio changu.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Kisha Isaya mwana wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, akisema: Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu umeniomba juu ya Saniharibu mufalme wa Asuria,


Kisha neno la Yawe lilimufikia Isaya kusema hivi:


Wewe umenisikia nikikulilia: Usiache kusikiliza maombi yangu ya musaada.


‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ ” Yesu akaendelea kuwaambia: “Mungu si Mungu wa waliokufa, lakini ni Mungu wa wanaokuwa wazima.”


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


na kuniambia: ‘Paulo, usiogope! Sherti usambe mbele ya Mufalme wa Roma. Na tena kwa kuwa inamupendeza Mungu kukutendea mema, yeye ataokoa maisha ya watu hawa wote wanaosafiri pamoja nawe.’


Lakini Mungu anayefariji watu wanyenyekevu, ametufariji kwa njia ya kufika kwa Tito.


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ