Isaya 38:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20025 Kwenda umwambie Hezekia kwamba: Mungu wa baba yako Daudi, anasema hivi: Nimesikia ombi lako na nimeyaona machozi yako. Basi, ninakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Kwa hiyo, sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba vilevile utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu mumoja wa uzao wako kwa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako watakuwa waangalifu juu ya mwenendo wao mbele yangu kama wewe ulivyofanya mbele yangu.’
Katika mwaka wa ine wa utawala wake, mufalme Yosia, akiwa bado kijana, alianza kumwabudu Mungu wa Daudi, babu yake. Kisha alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili alianza kusafisha inchi ya Yuda na Yerusalema kwa kuharibu pahali pa kutambikia miungu mingine, sanamu za Ashera, na sanamu zingine za kuchonga na za kuyeyusha.