Usikilize wakati tunapokusihi, mimi mutumishi wako na watu wako Waisraeli ambao tutaomba tukielekea pahali hapa. Kutokea kwako mbinguni, usikilize. Na ukisha kusikiliza, utusamehe.
Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.
akisema: Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote, na kutenda mazuri mbele yako. Hezekia akalia kwa uchungu sana.
Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.