Usikie maombi yangu, ee Yawe, usikilize kilio changu, usikae kimya ninapolia. Maana, mimi ni kama mugeni tu anayepita, ni musafiri kama vile babu zangu wote walivyokuwa.
Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Mutu hawezi kuishi kwa mukate tu, lakini kwa njia ya kushika kila neno Mungu analosema.’ ”
Aliwazarau akawaacha muone njaa na kisha akawapa mana mukule, chakula ambacho hamukukijua, wala babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hivyo kusudi apate kuwafundisha kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno Yawe analosema.
Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?