14 Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu!
Ee Mungu, ujitoe mwenyewe kuwa rehani kwa ajili yangu maana hakuna mwingine wa kujitoa kwa ajili yangu.
Kwa kilio nimekuwa ndugu ya imbwa wa pori, kati ya mimi na mbuni hakuna tofauti.
Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Ninauliza: “Utakuja wakati gani kunifariji?”
Ee Yawe, unijibu haraka; maana roho yangu imeregea kabisa! Usinigeuzie mugongo, kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.
Ee Mungu, tega sikio usikie maombi yangu; usiangalie pembeni ninapokuomba.
Ninazama ndani ya matope mengi, hakuna pahali pa kuweka miguu. Nimetumbukia kwenye shimo refu la maji, ninachukuliwa na maji mengi.
Tunanguruma kama dubu, tunaomboleza kama njiwa. Tunatazamia watu wanaofuata sheria ya Mungu, lakini hakuna, tunatazamia wokovu, lakini uko mbali nasi.
Tulichoka kukaa macho kungojea musaada; tulikesha na kungojea kwa hamu taifa ambalo halikuweza kutuokoa.
Ikiwa kuna watu walioponyoka, watakimbilia kwenye milima kama njiwa waliotishwa katika bonde. Kila mumoja wao ataomboleza kwa ajili ya zambi zake.
Vikingio vya mito vimefunguliwa, nyumba ya kifalme imejaa hofu.
Muji uko wazi kabisa, watu wamekamatwa mateka. Wanawake wake wanaomboleza, wanalia kama njiwa, na kujipigapiga kwenye vifua.
Kwa sababu ya kiapo hiki, Yesu amekuwa kihakikisho kwetu cha agano linalokuwa zuri zaidi.