Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 37:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 37:4
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Labda Yawe ataangalia mateso yangu, naye atanilipa wema kwa laana hii ninayopata leo.”


Basi, Yawe akawakasirikia sana watu wa Israeli na kuwafukuza kabisa mbele yake; hakuacha mutu isipokuwa kabila la Yuda peke yake.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”


Kwa maana Yawe alinyenyekeza inchi ya Yuda kwa ajili ya Ahazia mufalme wa Israeli sababu yeye alifanya uasherati katika Yuda na kumwasi Yawe.


“Mwende mutafute shauri kutoka kwa Yawe kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu ambao wamebaki katika Israeli na Yuda, juu ya maneno yanayokuwa katika kitabu kilichopatikana. Kwa sababu kasirani ya Yawe imetuangukia maana babu zetu hawakushika Neno la Yawe wala kufanya yaliyoandikwa humo.”


Mungu alisema atawaangamiza watu wake, lakini Musa, muchaguliwa wake, aliingilia kati, akazuia hasira yake isiwaangamize.


Umefanya hayo yote nami nimenyamaza. Unazani kwamba mimi ni kama wewe? Lakini sasa nitakukaripia, nitakugombeza waziwazi.


Sayuni umeachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kibanda cha mulinzi katika shamba la maboga, kama muji uliozungukwa kwa vita.


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Siku ile wazao wa Yakobo watakaobaki, ni kusema Waisraeli watakaopona hawatalitegemea tena taifa lililowaazibu, lakini watamutegemea kabisa Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tu.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Kisha huyo jemadari akasimama, akalalamika na kusema kwa luga ya Kiebrania: “Musikilize maneno ya mufalme mukubwa, mufalme wa Asuria!


Musimusikilize Hezekia anapowadanganya akisema: ‘Yawe atatuokoa.’ Kuna yoyote kati ya miungu ya mataifa aliyeokoa inchi yake toka katika mikono ya mufalme wa Asuria?


Ni nani kati ya miungu ya inchi hizi aliyeokoa inchi zao toka katika mikono yangu. Yawe ataweza kuuokoa Yerusalema?”


Ee, Yawe, fungua macho uone, tega sikio lako uyasikie matusi yote ambayo Saniharibu amepeleka na kukutukana wewe Mungu Mwenye Uzima.


Wale watakaobaki katika ukoo wa Yuda wataongezeka na kuwa wengi kama vile muti unavyotoa mizizi yake katika udongo na kuzaa matunda juu.


Maana kutakuwa watu watakaobaki kule Yerusalema; kule kwenye mulima Sayuni kutakuwa watu wachache watakaobakia. Yawe wa majeshi amekusudia kukamilisha hayo.


Basi, hao watumishi wa mufalme Hezekia walipokwisha kufika kwa Isaya,


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Musikilize, enyi wazao wa Yakobo, munisikilize, enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli. Mimi niliwatunza ninyi tangu mulipozaliwa; niliwabeba ninyi tangu katika tumbo la mama yenu.


Hezekia, mufalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda hawakumwua Mika. Hezekia alimwogopa Yawe na kuomba rehema kwake. Naye Yawe akabadilisha nia yake ya kuleta hasara aliyokusudia juu yao. Lakini sisi tuko mbio kwa kujiletea hasara wenyewe.


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Aliwaambia wamwombe Mungu wa mbinguni awaonee huruma juu ya fumbo hilo, kusudi wao wasiangamie pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.


Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Niliwaona nzige hao wakikula na kumaliza kila jani katika inchi. Halafu nikasema: Ee Bwana wetu Yawe, ninakusihi utuhurumie! Wazao wa Yakobo wataweza kuishi namna gani? Wao ni wadogo sana!


Isaya alisema kwa sauti juu ya Waisraeli: “Ijapokuwa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaookolewa.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Sasa ninaomba unipe inchi hii ya milima ambayo Yawe aliniahidi siku ile. Wewe ulisikia siku ile kwamba Waanaki waliishi humo katika miji yenye kuta; labda Yawe atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza kama vile Yawe alivyosema.”


Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


Daudi akawauliza wale waliokuwa karibu naye: “Mutu atakayemwua Mufilistini huyu na kuikomboa Israeli kutokana na haya hii atafanyiwa nini? Ni nani huyu Mufilistini, mutu mupagani, anayesubutu kuwatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima?”


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


Basi, wakamwambia Samweli: “Usiache kumulilia Yawe, Mungu wetu, kwa ajili yetu. Endelea kumulilia atuokoe kutokana na Wafilistini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ