Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 37:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Umewatuma watumishi wako kumuchekelea Bwana wenu; wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita, nimefika juu kwenye vichwa vya milima, mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni. Nimeangusha mierezi yake mirefu, na misunobari mizurimizuri. Nimevifikia vichwa vyake na ndani ya pori zake kubwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 37:24
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Adui akajisemesha: ‘Nitawafuata na kuwakamata; nitagawanya vitu mpaka hamu yangu iishe. Tutafuta upanga wetu, tutawaangamiza kwa mukono wetu.’


Pori yake yenye utukufu na mashamba yake mazuri, Yawe atayaangamiza yote; itakuwa kama mutu aliyemalizika na ugonjwa.


Bwana, Yawe wa majeshi atakata matawi kwa ukali, miti mirefu itaangushwa chini, wanaokuwa juu watashushwa.


Atakata vichaka vya pori kwa shoka; Lebanoni na mierezi yake yenye utukufu itaanguka.


Miti ya shindano inafurahia kuanguka kwako, nayo mierezi ya Lebanoni pamoja inasema: Kwa vile sasa umeangushwa, hakuna mukata miti atakayekuja juu yetu!


Bado kidogo tu, pori la Lebanoni litageuzwa kuwa shamba lenye udongo muzuri, na shamba lenye udongo muzuri kuwa pori.


Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Yawe anasema hivi juu ya nyumba ya kifalme ya Yuda: Ingawa unaonekana vizuri kama inchi ya Gileadi, kama vichwa vya milima ya Lebanoni, ninaapa kwamba nitakufanya kuwa jangwa, ukuwe muji usiokaliwa na watu.


Nitawatayarisha waangamizaji wakufikie, kila mumoja akishika silaha yake. Watazikata nguzo zako nzuri za mierezi, na kuzitumbukiza katika moto.


Misri ni kama muto Nili uliofurika, kama mito inayovumisha mawimbi. Ilisema: Nitajaa, nitaifunika inchi, nitaiharibu miji na wakaaji wake.


Wewe mwanadamu, geukia upande wa kusini, uhubiri juu ya inchi ya kusini, juu ya wakaaji wa pori la Negebu.


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ