Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 37:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 basi huu ndio ujumbe wa Yawe juu ya huyo mufalme: Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa, Watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 37:22
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hili ndilo neno Yawe alilosema juu yake: “Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa, watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.


Kama mungekuwa mimi, na mimi ninyi, ningeweza kusema kama ninyi. Ningeweza kutunga maneno juu yenu, na kutikisa kichwa changu.


Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.


Ee Yawe, wewe unayeniopoa kutoka nguvu za kifo, uangalie mateso wale wanaonichukia wanayoniletea na kunirehemu


Sayuni umeachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kibanda cha mulinzi katika shamba la maboga, kama muji uliozungukwa kwa vita.


Leo hii, adui atapiga kambi kule Noba, anainua mukono wake kwa mulima Sayuni, kilima cha Yerusalema.


Alisema: Ewe binti Sidona, hautaweza kufanya sherehe tena; hata ukikimbilia Kipuro, kule nako hautapata pumziko!


Shuka, uikae katika mavumbi, ewe bikira, binti wa Babeli! Ikaa chini pasipo kiti cha kifalme, ewe binti wa Wakaldea! Tokea sasa hautaitwa tena murembo wala mwenye kupendeza.


Yawe ametangaza katika dunia yote, muwaambie watu wa Sayuni hivi: Mukombozi wenu anakuja, yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Hivi ndivyo utakavyowaambia: Heri macho yangetoa machozi usiku na muchana, wala yasikome kutiririka, maana, watu wangu wamepata hasara kubwa, wameumizwa kidonda kikubwa sana.


Wameifanya inchi yao kuwa kitisho, kuwa kitu cha kuzomewa siku zote. Kila mutu anayepita huko anashangaa na kutikisa kichwa chake.


Yawe aliwakataa waaskari walionilinda, alitangaza wakati kamili wa kuniazibu kuwaponda vijana wangu wanaume. Aliwaponda kama katika kikamulio, watu wangu wa Yuda.


Nikuambie nini, ee Yerusalema? Nikulinganishe na nini? Nikufananishe na kitu gani kusudi niweze kukufariji, ee Sayuni uliyekuwa muzuri? Maangamizi yako ni mengi kama bahari, ni nani atakayekuponyesha?


Wapita njia wote wanakuchekelea; wanakupigia muunzi, ee Yerusalema, wakitikisa vichwa vyao kwa mazarau na kusema: Huu ndio ule muji uliofikia ukamilifu wa uzuri, muji uliokuwa furaha ya dunia nzima?


Umeanguka na hautainuka tena ewe binti Israeli! Umeachwa ukiwa katika inchi yako, hakuna hata mutu wa kukuinua.


Imba kwa sauti, ewe Sayuni, piga vigelegele, ee Israeli. Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalema!


Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


“Muwaambie wakaaji wa muji Sayuni: ‘Angalia, mufalme wenu anakuja kwenu. Yeye ni munyenyekevu, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, kitoto cha punda.’ ”


Watu waliokuwa wakipita pale walimutukana, na kutikisatikisa vichwa vyao,


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ