Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 37:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 37:20
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

usikilize kutokea kwako mbinguni. Umujalie yule mugeni yote atakayokulilia, kusudi watu wote katika ulimwengu wapate kujua jina lako na kukutii kama watu wako Waisraeli wanavyofanya, na wapate kufahamu kwamba nyumba hii ambayo nimeijenga, inajulikana kwa jina lako.


Basi, maneno yangu haya ambayo ni ombi langu mbele ya Yawe, yakuwe karibu na Yawe, Mungu wetu, muchana na usiku, naye amujalie mutumishi wake, na watu wake Waisraeli, kusudi wafanikiwe katika mahitaji yao ya kila siku.


Nayo mataifa yote katika ulimwengu yatajua kwamba kweli Yawe ndiye Mungu wala hakuna mwingine.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Wao wanatenda zambi katika masemi yao yote, kwa hiyo wanaswe katika kiburi chao! Kwa sababu ya laana na uongo wao,


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


“Ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine; hakuna Mungu mwingine lakini mimi. Ninakuimarisha ingawa wewe haunijui,


Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.


Yawe akaniambia hivi: Nitaonyesha utukufu wangu kwa mataifa yote, na kuwaonyesha jinsi ninavyotumia nguvu yangu kwa kutimiza hukumu zangu za haki.


Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ