Isaya 37:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.
Walipomwita mufalme Hezekia walipokelewa na Eliakimu mwana wa Hilkia ambaye alikuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa mwandishi wa mufalme, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wa habari.
Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna mwandishi, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.
Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”
Mordekayi alipojua yote yaliyotukia, akapasua nguo zake, akavaa nguo ya gunia, na kujitia majivu. Kisha, akapita katikati ya muji akilia kwa sauti ya uchungu.
Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.
Miaka mitatu mbele ya pale, Yawe alimwambia Isaya mwana wa Amozi hivi: Kwenda uvue nguo ya gunia uliyokuwa umevaa katika kiuno, na viatu vyako. Isaya akafanya kama alivyoambiwa; akakuwa anatembea uchi na bila viatu.
Nao walikutana na Eliakimu mwana wa Hilkia, aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, aliyekuwa katibu, pamoja na mwandishi Yoa mwana wa Asafu.
Kisha Isaya mwana wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, akisema: Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu umeniomba juu ya Saniharibu mufalme wa Asuria,
Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.
Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.