Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 37:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Walitupa miungu yao katika moto kwa sababu haikukuwa miungu ya kweli, lakini sanamu za miti na mawe zilizochongwa na mikono ya watu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 37:19
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wafilistini waliziacha sanamu zao za miungu pahali pale, naye Daudi na watu wake wakazikamata.


Basi, akamutwaa yule mwana-ngombe akamuchoma kwa moto, akamusaga mpaka akakuwa unga, akakoroga unga huo katika maji na kuwalazimisha Waisraeli wakunywe.


Lakini Asuria hakuwazia hivyo, yeye alikuwa na nia ingine; alikusudia kuharibu kabisa, kuangamiza mataifa mengi sana.


Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.


Inchi yao imejaa sanamu za miungu, watu wake wanaabudu kazi ya mikono yao, vitu walivyotengeneza wao wenyewe.


Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaazibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.


Hakika, ninyi si kitu kabisa. Hamuwezi kufanya kitu chochote. Anayechagua kuwaabudu ninyi ni chukizo.


Miungu hiyo yote ni udanganyifu, haiwezi kufanya kitu chochote; sanamu zao ni upepo tu, hazina maana.


Fundi anamusaidia mufuaji wa zahabu. Naye anayelainisha sanamu kwa hama, anamusaidia anayeiunga kwa misumari. Wote wanasema: Ni vizuri sana! Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.


Sehemu iliyobaki ya muti huohuo, anajichongea nayo mungu, anajifanyia sanamu yake, kisha anapiga magoti mbele yake na kuiabudu. Wanaomba mbele yake wakisema: Wewe ni mungu wangu, uniokoe!


Nami nitawahukumu Waisraeli kwa ajili ya uovu wao wote, kwa maana waliniacha mimi na kuifukizia miungu mingine ubani na kuabudu sanamu walizojitengenezea wenyewe.


Basi, utawaambia hivi: Miungu hiyo ambayo haikuumba mbingu na dunia itaangamia. Itatoweka kabisa toka katika dunia, hapa chini ya mbingu.


Mwanadamu anaweza kujitengenezea miungu? Kweli hiyo si miungu hata kidogo!


Kuna taifa ambalo limekwisha kubadilisha miungu yao ingawa miungu hiyo si miungu? Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao, wakafuata miungu isiyokuwa na faida yoyote.


Atabeba sanamu za miungu yao na vyombo vya bei kali vya feza na zahabu mpaka katika inchi ya Misri. Kwa muda wa miaka michache, mufalme wa kusini hatamushambulia mufalme wa kaskazini.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Zamani, mulipokuwa hamumujui Mungu, mulikuwa watumwa wa miungu isiyokuwa ya kweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ