Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 37:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 “Ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 37:16
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.


Nalo jina lako litatukuzwa milele, nao watu watasema: ‘Yawe wa majeshi ni Mungu juu ya Israeli!’ Na jamaa yangu, mimi Daudi mutumishi wako, itaimarika mbele yako.


Kwa mawe hayo, Elia alimujengea Yawe mazabahu. Akachimba mufereji pembenipembeni ya mazabahu hiyo, mufereji ambao unaweza kujazwa na maji yapata litre kumi na ine.


Kisha makuhani wakaliingiza Sanduku la Agano la Yawe kwa nafasi yake katika chumba cha ndani cha nyumba, ni kusema Pahali Patakatifu Sana, chini ya mabawa ya makerubi.


Halafu akarudi kwa mutu wa Mungu pamoja na watu wake, akasema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote katika dunia lakini tu Mungu wa Israeli; kwa hiyo, tafazali sasa upokee zawadi ya mutumishi wako.”


Basi sasa, kila mutu kati yenu ninyi wote munaokuwa watu wake, Mungu wake akuwe naye na aende katika Yerusalema huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yawe, Mungu wa Israeli, Mungu anayeabudiwa kule Yerusalema.


aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao. Yeye anashika ahadi yake milele.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


Wewe ndiwe mukubwa, unafanya maajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.


Yawe anatawala, mataifa yanatetemeka! Ameikaa juu ya makerubi, nayo dunia inatikisika!


Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Dunia iliumbwa na yule anayeikaa juu ya mbingu; kutoka huko wakaaji wa dunia ni kama mapanzi! Yeye ametandika mbingu kama pazia, na kuzikunjua kama hema la kuishi ndani yake.


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Yawe ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu katika dunia. Yeye haregei hata kidogo wala kuchoka. Maarifa yake hayachunguziki.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu na kuzitandika kama hema, aliyeifanya dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, anayewapa watu wanaokaa ndani yake uzima, na kuwajalia uzima wote wanaoishi ndani yake:


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Ni mimi niliyeifanya dunia, na kuumba mwanadamu anayeishi humo. Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu, na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.


Munigeukie mimi mupate kuokolewa, popote munapokuwa katika dunia. Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake.


Munitambue mimi peke yangu, Yawe wa majeshi, kuwa mutakatifu. Muniogope na kuniabudu mimi peke yangu.


Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, wala hakuna hata kitu kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


Kwa njia yake, Mungu aliumba vitu vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia, vyenye kuonekana na visivyoonekana; ikiwa ni ufalme, ukubwa, utawala au mamlaka. Mungu aliumba vyote kwa njia yake na kwa ajili yake.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Kwa hiyo, walituma watumishi kule Shilo, nao wakalileta Sanduku la Agano la Yawe wa majeshi ambaye anatawala juu ya makerubi. Wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi walikuja pamoja na lile Sanduku la Agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ