Beni-Hadadi akamutumia Ahabu ujumbe huu: “Miungu iniue ikiwa kule Samaria kutabakia mavumbi ya kutosha kwa kujaza vitanga vya mikono kwa kila mumoja wa watu wangu wengi wanaonifuata!”
Alitwaa zahabu yote na feza, hata na vifaa vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe na katika hazina ya nyumba ya kifalme. Vilevile alibeba mateka, kisha akarudi Samaria.
Kisha mufalme wa Asuria alimutuma jemadari kutoka Lakisi na kundi kubwa kumwendea mufalme Hezekia. Jemadari yule alisimama karibu na mufereji wa birika linalokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea shamba la wafuaji wa nguo.
Lakini hata kama mukiniambia ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?
Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.