Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 36:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Halafu yule jemadari wa Asuria aliwaambia: “Mumwambie Hezekia kwamba mufalme mukubwa wa Asuria anamwuliza: Unategemea nini kwa kukazana kwako?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 36:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha mufalme wa Asuria alimutuma majemadari wakubwa watatu pamoja na kundi kubwa la waaskari kutoka Lakisi kwenda kwa mufalme Hezekia kule Yerusalema. Walisafiri na kufika Yerusalema. Nao walipofika waliingia na kusimama karibu na mufereji wa kisima kinachokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea kiwanja cha mufuaji wa nguo.


Hezekia alimutegemea Yawe, Mungu wa Israeli; hakuna aliyekuwa kama yeye kati ya wafalme wa Yuda waliomufuata au waliomutangulia.


“Mumwambie Hezekia mufalme wa Yuda: ‘Usikubali Mungu wako unayemutegemea akudanganye kwa kukuahidi kwamba Yerusalema hautatekwa na mufalme wa Asuria.


Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”


Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima. Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Namna gani munaweza kusema: Sisi ni mashujaa, na watu wenye nguvu nyingi za vita?


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ