Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 36:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Musimusikilize Hezekia anapowadanganya akisema: ‘Yawe atatuokoa.’ Kuna yoyote kati ya miungu ya mataifa aliyeokoa inchi yake toka katika mikono ya mufalme wa Asuria?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 36:18
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya, na ndimi hizo zinazojigamba.


Basi nitashindwa kuutendea Yerusalema na sanamu zake, kama nilivyoutendea Samaria na sanamu zake?


Lakini Asuria hakuwazia hivyo, yeye alikuwa na nia ingine; alikusudia kuharibu kabisa, kuangamiza mataifa mengi sana.


Zaidi ya hayo, munafikiri nimekuja bila amri ya Yawe kwa kuishambulia na kuiangamiza inchi hii? Yawe ndiye aliyeniambia: ‘Ushambulie inchi hii na kuiangamiza!’ ”


Musikubali awashawishi kusudi mumutegemee Yawe, akisema: ‘Yawe atatuokoa na muji huu hautatiwa katika mikono wa mufalme wa Asuria.’


mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika inchi kama hii yenu, inchi yenye ngano na divai, inchi yenye mukate na mashamba ya mizabibu.


Lakini hata kama mukiniambia ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?


“Mumwambie Hezekia mufalme wa Yuda: Usikubali Mungu wako unayemutegemea akudanganye kwa kukuahidi kwamba Yerusalema hautatekwa na mufalme wa Asuria.


Wewe umekwisha kusikia jinsi wafalme wa Asuria walivyotendea inchi nyingine na kuziangamiza kabisa. Unazani wewe utaokoka?


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Kwa hiyo, ulirefuka sana kupita miti yote katika pori; matawi yake yalizidi kuwa mengi na makubwa, kutokana na maji mengi ndani ya mizizi yake.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ