Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 34:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mbogo wataangamizwa pamoja nao, wana-ngombe pamoja na ngombe dume. Inchi italewa na damu, udongo utashiba kwa mafuta yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 34:7
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uokoe nafsi yangu toka upanga, uokoe maisha yangu toka mikono ya imbwa hao!


Kutoka katika hekalu lako, Yerusalema, ambapo wafalme watakufikia na zawadi zao,


Hao waadui zako, ee Yawe, hao waadui zako, hakika wataangamia; wote wanaotenda maovu, watatawanyika!


Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.


Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.


Hata waaskari wake wa mushahara ni kama wana-ngombe wanono; nao tena wamegeuka, wakakimbia pamoja, wala hawakuweza kuvumilia, kwa maana siku yao ya kuangamizwa imefika, wakati wao wa kuazibiwa umetimia.


Enyi wanyanganyi wa mali yangu, ijapokuwa munafurahi na kushangilia, munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano, na kulia kama farasi dume,


Muwaue waaskari wake hodari; muache washukie kwenye machinjo. Ole kwao, maana siku yao imetimia, wakati wao wa kuazibiwa umefika!


Nitaikunywesha inchi damu yako mpaka juu ya milima, mashimo yatajaa damu yako.


Sasa, ewe mwanadamu, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Uite ndege wote na nyama wote wa pori wakusanyike toka pande zote na kuja kukula karamu ya sadaka ya nyama ninayowatayarishia, ambayo itakuwa kubwa sana juu ya milima ya Israeli, ambako watakula nyama na kunywa damu.


Watakula nyama ya mashujaa, watakunywa damu ya wakubwa wa dunia watakaochinjwa kama kondoo dume au wana-kondoo, mabeberu au ngombe dume wanono wa Basani.


Mungu aliyewatoa kutoka Misri, anawapigania kwa nguvu kama za mbogo.


Mungu aliwaondoa kutoka Misri, naye anawapigania kwa nguvu kama mbogo. Atayateketeza mataifa yanayokuwa waadui zao, atavunjavunja mifupa yao, atawachoma kwa mishale yake.


Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza, pembe zake ni za mbogo dume. Atazitumia kusukuma mataifa; yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia. Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi na Manase kwa maelfu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ