Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 34:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 34:2
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, anawakaripia kwa kasirani na kuwatisha kwa hasira, akisema:


Wachawi wa Misri, kwa uchawi wao, wakajaribu kuyageuza mavumbi yakuwe chawa, lakini hawakuweza. Chawa wale wakaenea juu ya watu na nyama.


Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!


Wanakuja kutoka inchi za mbali, wanatoka hata miisho ya dunia: Yawe na silaha za hasira yake anakuja kuiangamiza dunia.


Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.


Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu, mujifungie humo ndani. Mujifiche kwa muda mufupi, mpaka kasirani ya Yawe ipite.


Wakati utakapofika ambapo waadui watauawa na minara yao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mulima na kilima.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.


Nimewapangia kifo kwa upanga, ninyi wote mutanaswa kwa kuchinjwa! Maana, nilipowaita, hamukuniitikia; niliposema, hamukunisikiliza. Mulitenda maovu mbele yangu, mukachagua yale nisiyoyapenda.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Yawe atatoa hukumu kwa moto atawaazibu watu wote kwa upanga; nao atakaowaangamiza watakuwa wengi.


Vishindo hivyo vitasikilika mpaka mwisho wa dunia, maana Yawe ana mashitaki juu ya mataifa; anawahukumu wanadamu wote, naye atawaua waovu kwa upanga! –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Hasara italifikia taifa kwa taifa, na zoruba itavuma kutoka miisho ya dunia.


Siku hiyo, wale watakaouawa na Yawe watasambaa kutoka upande mumoja wa dunia mpaka upande mwingine. Hakuna atakayeomboleza juu yao, wala maiti zao hazitakusanywa wala kuzikwa; zitabaki sawa mboleo juu ya udongo.


Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wivu wangu unawaka sana. Nitayaazibu mataifa mengine na hasa watu wa inchi ya Edomu. Wao kwa furaha ndani ya moyo na mazarau walikamata hiyo inchi inayokuwa yangu ikuwe yao.


Kwa hiyo muningojee mimi Yawe, ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki. Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme, kuyamwangia kasirani yangu, na ukali wa hasira yangu. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa kasirani yangu.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Tokea mbinguni Mungu anaonyesha kwamba anawakasirikia wote wanaofanya zambi na maovu, wanaowazuiza watu wasitambue ukweli kwa njia ya matendo yao mabaya.


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


Na mutu yeyote ambaye jina lake lililokosa kuandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.


Walitawanyika katika dunia yote, na kuzunguka kambi ya watu wa Mungu na muji wake alioupenda. Lakini moto ukashuka toka mbinguni, ukawateketeza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ