Wenye nguvu watakuwa kama majani yenye kukauka, matendo yao yatakuwa kama cheche za moto. Watateketea pamoja na matendo yao, wala hakutakuwa mutu wa kuwaokoa.
Hautakaliwa tena na watu hata kidogo, watu hawataishi humo katika vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayesimamisha hema yake humo, wala muchungaji atakayechunga nyama wake humo.
Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.
Kama vile Sodoma na Gomora na miji jirani yake ilivyoangamizwa, hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi Edomu wala kufanya mashauri humo. –Ni Yawe anayesema.–
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.