Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 33:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Enyi watu wa Yerusalema, Yawe atawajalia usalama, atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa. Akiba yenu kubwa ni kumwogopa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 33:6
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Kumwogopa Mungu si ndilo tegemeo lako? Na ukamilifu wa mwenendo wako si ndilo tumaini lako?


Ninamwambia Yawe: “Wewe ni Mungu wangu.” Usikilize, ee Yawe, sauti ya ombi langu.


Yawe ni nguvu ya watu wake; yeye ni kimbilio la mufalme aliyemuchagua.


Ujifungie upanga wako, ewe shujaa! Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka.


Mali ni taji ya utukufu wa wenye hekima, lakini ujinga ni kitambaa cha wapumbafu.


Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.


Kumwogopa Yawe ni chemichemi ya uzima inayowezesha mutu kuepuka mitego ya kifo.


Afazali kuwa na kidogo na kumwogopa Yawe, kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.


Kumwogopa Yawe kunaongoza kwenye uzima; anayemwogopa anajaliwa pumziko la kutoshelea, wala hatapatwa na ubaya wowote.


utaelewa maana ya kumwogopa Yawe, utafahamu maana ya kumujua Mungu.


Taifa lenye fujo lina viongozi wengi, lakini kwa kiongozi mumoja mwenye akili na maarifa kuna utengemano.


Mufalme akifuata sheria ya Mungu, anaimarisha inchi. Lakini akipenda kituliro, taifa linaangamia.


Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.


Hekima inamufanya mwenye hekima kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi katika muji.


Katika mulima mutakatifu wa Mungu hakutakuwa ubaya wala uharibifu. Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi, kama vile maji yanavyojaa katika bahari.


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Kutokana na kutenda kwa haki, watu watapata amani, utulivu na usalama kwa milele.


Watu wangu watakaa katika makao ya amani, katika pahali penye usalama na nafasi yenye utulivu.


Muangalie Sayuni tunamofanyia sikukuu zetu; muangalie Yerusalema, makao matulivu, hema imara; misumari yake haitaongolewa hata kidogo, kamba zake hazitakatwa hata moja.


Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe, litapata wokovu wa milele. Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.


Wafungwa watafunguliwa upesi, hawatakufa na kushuka katika shimo, wala hawatakosewa chakula.


Muinue macho, muangalie mbingu, kisha muangalie dunia kule chini. Mbingu zitatoweka kama moshi, dunia itachakaa kama nguo, na wakaaji wake watakufa kama vidudu. Lakini wokovu ninaouleta unadumu milele; ukombozi wangu hautakoma hata kidogo.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Utukufu wa Yawe utaenea pote katika dunia, kama vile maji yanavyoenea katika bahari.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


tunahuzunishwa lakini tunafurahi siku zote. Tunaonekana kama wamasikini lakini tunatajirisha watu wengi, hatuna kitu, lakini tunakuwa na vitu vyote.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


Hakika, dini ni pato kubwa kwa mutu kama anafurahia vitu anavyokuwa navyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ