Likaharibu miji yote iliyokuwa kandokando ya Gerari, kwa kuwa watu waliokuwa katika miji ile, walipatwa na hofu ya Yawe. Likabeba mali nyingi kutoka katika miji ile, kwa sababu kulikuwa mali mengi sana.
Yosafati na waaskari wake wakaenda kukamata vitu. Wakakuta ngombe wengi, mali, nguo na vitu vingine vya bei kali. Iliwachukua muda wa siku tatu kusomba vitu hivyo, na hata hivyo, hawakuvimaliza maana vilikuwa vingi sana.
Ewe Sayuni, kamba zako zimeregea, haziwezi kushikilia matanga yake, wala kufungia paa zao. Lakini vitu vingi vilivyonyanganywa vitagawanywa; hata vilema wataweza kupata sehemu yao.
basi, mimi nimeunyoosha mukono juu yenu kwa kuwaazibu; nitawaacha mukamatwe mateka na watu wa mataifa mengine. Nitawaangamiza kabisa, nanyi hamutakuwa taifa tena wala kuwa na inchi. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
Nzige, makundi kwa makundi, wameishambulia mimea; kilichoachwa na nzige kimekuliwa na tunutu, kilichoachwa na tunutu kimekuliwa na parare, kilichoachwa na parare kimeliwa na panzi.
Kama vile moto unavyoteketeza, Jeshi hilo linaharibu kila kitu mbele yake na kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa; mbele ya kupita kwao, inchi ni kama bustani ya Edeni, lakini wakisha kupita, ni jangwa tupu. Hakuna kinachoweza kuponyoka!