Basi, wewe Yeremia utatabiri maneno haya yote juu yao, na kusema hivi: Yawe atanguruma kutoka juu, atatoa sauti yake kutoka kwenye makao yake matakatifu; atanguruma kwa nguvu kwa ajili ya watu wake, atapiga kelele kama wenye kukamua zabibu, kwa ajili ya wakaaji wote wa dunia.
Vishindo hivyo vitasikilika mpaka mwisho wa dunia, maana Yawe ana mashitaki juu ya mataifa; anawahukumu wanadamu wote, naye atawaua waovu kwa upanga! –Ni ujumbe wa Yawe.