Abrahamu akakubaliana na Efuroni, akamupimia kadiri ya feza alizotaja mbele ya Wahiti wote, feza vikoroti mia ine, kadiri ya vipimo vya wachuuzi wa wakati ule.
Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.
Hezekia akatuma ujumbe kwa Saniharibu kule Lakisi na kumwambia: “Nimefanya makosa. Tafazali, uache kunishambulia, nami nitalipa chochote unachotaka.” Mufalme wa Asuria akaagiza Hezekia amuletee kilo elfu kumi za feza na kilo elfu moja ya zahabu.
Musimusikilize Hezekia, maana mufalme wa Asuria anasema: ‘Mukuwe na amani nami na kujitoa kwangu. Kisha kila mumoja wenu ataweza kula matunda ya mizabibu yake mwenyewe na matunda ya tini yake mwenyewe na kunywa maji ya kisima chake mwenyewe,
mateso na taabu yangu. Unajua mambo yote ambayo yalinitokea kule Antiokia, Ikonio na Listra. Mateso haya niliyavumilia, na Bwana akaniokoa katika yote.
Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.