Mungu anayekuwa mwangaza wa Israeli atakuwa kama moto. Mutakatifu wa Israeli atakuwa ulimi wa moto ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu, miiba yake na michongoma zake pamoja.
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Moabu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamemukosea heshima marehemu mufalme wa Edomu kwa kuichoma mifupa yake kwa moto kwa kujitengenezea chokaa!