Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 32:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kutokana na kutenda kwa haki, watu watapata amani, utulivu na usalama kwa milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 32:17
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Barua ile iliandikwa kwa Wayuda wote, na mifano ya barua zile kupelekewa katika majimbo yote mia moja makumi mbili na saba ya ufalme wa Ahasuero. Barua ile iliwatakia Wayuda amani na usalama,


Wanaopenda sheria yako wana amani kubwa; hakuna kinachoweza kuwaangusha.


Hakika yeye ni tayari kuwaokoa wanaomuheshimu, na utukufu wake utadumu katika inchi yetu.


Utuonyeshe wema wako, ee Yawe, utujalie wokovu wako.


Lakini mutu anayenisikiliza atakaa salama, atatulia bila kuogopa mabaya.”


Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Wivu wa Efuraimu juu ya Yuda utakoma, hakutakuwa tena uadui kati ya Yuda na Efuraimu.


Ee Mungu, unawaweka katika amani wanaokuwa imara, unawaweka katika amani kwa sababu wanakutegemea.


Yeye alikuwa amewaahidia ninyi: Nitawaonyesha ninyi pumziko, nitawapa pumziko enyi muliochoka. Hapa ni pahali pa pumziko. Lakini wao hawakutaka kunisikiliza.


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Enyi watu wa Yerusalema, Yawe atawajalia usalama, atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa. Akiba yenu kubwa ni kumwogopa Yawe.


Ingekuwa heri ungalizitii amri zangu! Halafu baraka zingekutiririkia kama muto, ungefanikiwa kwa wingi kama mawimbi ya bahari.


Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.


Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.


Maana Yawe anasema hivi: Nitakuletea fanaka nyingi kama muto, utajiri wa mataifa kama muto uliofurika. Nanyi mutanyonya na kubebwa kama mutoto muchanga, mutabembelezwa kama mutoto juu ya magoti ya mama yake.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Maadibisho yoyote wakati yanapotolewa yanaonekana kama ni tendo la huzuni wala si la furaha. Lakini kwa mwisho yanawaletea wale waliofundishwa nayo, maisha ya amani na ya haki.


Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.


Hivi upendo umekamilishwa ndani yetu, kusudi tupate kuwa na tumaini kwa Siku ile ya hukumu. Kwa sababu maisha yetu katika dunia hii yanafanana na maisha ya Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ