Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 32:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 32:15
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ukiwapulizia pumzi yako, wanaumbwa; wewe unafanya vitu vipya katika dunia.


Mungu aligeuza mito kuwa jangwa, chemichemi akazikausha kabisa.


Aligeuza jangwa kuwa ziwa, na inchi ya kukauka kuwa chemichemi za maji.


Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.


Atawaongoza waamuzi wa tribinali kuhukumu kwa haki, nao walinzi wa muji atawapa nguvu.


Bado kidogo tu, pori la Lebanoni litageuzwa kuwa shamba lenye udongo muzuri, na shamba lenye udongo muzuri kuwa pori.


Muchanga wa moto katika jangwa utakuwa ziwa la maji, inchi kavu itabubujika vijito. Makao ya imbwa wa pori yatajaa maji; nyasi zitaota na kukomaa kama mianzi.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Enyi mbingu, munyeshe umande kutoka kule juu, mawingu yatiririshe ushindi; dunia ifuguke, ichipushe wokovu, na kuotesha haki vilevile! Mimi, Yawe nimefanya hayo.


Toka magaribi mpaka mashariki, kila mutu atamwogopa Yawe na kutambua utukufu wake. Maana atakuja kama muto wenye kuporomoka mbio, muto unaosukumwa kwa upepo wa Yawe.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Nitatia Roho yangu ndani yenu, nanyi mutaishi, nami nitawaweka katika inchi yenu wenyewe. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi Yawe nimesema, nami nitafanya hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Na mimi mwenyewe nitawatumia zawadi ile Baba yangu aliyoahidi ishuke juu yenu. Lakini mungojee kule Yerusalema mpaka mutakapojazwa uwezo kutoka juu.”


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


Basi si zaidi sana matokeo ya utumishi wa Roho yatakuwa yenye utukufu?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ