Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 32:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mutetemeke kwa woga, enyi munaojiikalia tu; mutetemeke kwa hofu, enyi munaostarehe! Muvue nguo zenu, mubakie uchi, mujifungie nguo ya gunia katika viuno vyenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 32:11
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tumeshiba muda murefu mazarau ya watajiri, nayo masimango ya wenye kiburi.


Watu wakalia waliposikia habari hizi mbaya, wala hakuna aliyevaa mapambo yake.


Wanapita katika njia wakivaa magunia. Kwenye paa za nyumba na viwanja vya muji watu wanalia na kukauka kwa machozi.


Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


Nao wataingia katika mapango chini ya mawe na kwenye nyufa za mawe, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Kwa pahali pa harufu ya marasi watatoa uvundo; kwa pahali pa mikaba mizuri watatumia kamba; kwa pahali pa nywele nzuri watakuwa na upaa; kwa pahali pa nguo nzuri watavaa magunia; uzuri wao wote utageuka kuwa haya.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Sasa, basi, sikiliza, ewe mupenda raha, wewe unayezani kuwa katika usalama, na kujisemesha: Mimi ndiye. Hakuna mwingine isipokuwa mimi. Sitakuwa mujane hata kidogo, wala sitakufiwa na watoto wangu.


Kwa hiyo, muvae gunia, muomboleze na kulia; kwa maana Yawe hajaondoa hasira yake kali kwenu.


Muomboleze, enyi watu wa Hesiboni, maana muji Ai umeharibika! Mulie, enyi wabinti wa Raba! Muvae magunia, muomboleze na kukimbia huko na huko ndani ya ukuta wenu! Maana mungu Milkomu atapelekwa katika uhamisho, pamoja na makuhani wake na watumishi wake.


Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.


Basi, muwaite wakaka zenu, “Watu wangu”, na wadada zenu, “Waliohurumiwa”.


Mulie kama vile binti aliyevaa gunia akiombolezea kifo cha muchumba wake.


Kwa hiyo, enyi Waisraeli, nitawaazibu. Na kwa sababu nitafanya jambo lile, mujitayarishe kwa kutana na Mungu wenu!


Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama, muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine! Jinsi gani umekuwa mutupu na makao ya nyama wa pori! Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Mumeishi katika utajiri na kujifurahisha katika maisha yenu katika dunia. Mumejinenepesha kwa kuwa tayari kwa siku ya kuchinjwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ