Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 31:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kama vile ndege anavyonyoosha mabawa juu ya vitoto vyake, ni vile Yawe atakavyolinda Yerusalema. Ataulinda na kuukomboa, ataukinga na kuuokoa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 31:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho wa Mungu alikuwa akitanda juu ya maji.


Kweli, kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi, nitaulinda na kuukoa muji huu.”


Kwa njia hii basi, Yawe akamwokoa mufalme Hezekia na wakaaji wa Yerusalema kutoka mukono wa Saniharibu mufalme wa Asuria, na kutoka mukono wa waadui zake wote. Akawapa maisha ya amani na wajirani zao wote.


Yawe anawasaidia na kuwaokoa; anawaopoa kutoka makucha ya waovu na kuwaokoa, maana wanakimbilia kwake.


Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.


Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupatia musaada kila asubui.


Atakufunika kwa mabawa yake; utapata usalama kwake. Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.


ninyi mutawajibu: ‘Hii ni sadaka ya Pasaka kwa Yawe, kwa sababu alipita nyumba za Waisraeli katika inchi ya Misri. Aliwaua Wamisri, lakini sisi hakutuua.’ ” Waisraeli wakainamisha vichwa na kumwabudu Yawe.


‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.


Kama mutu anayenyoosha mukono kwenye chicha, ndivyo nilivyokamata mali ya mataifa; kama mutu anayeokota mayai yaliyoachwa ndani ya chicha, ndivyo nilivyoyaokota katika dunia yote. Watu wote walikuwa sawa ndege ambaye hapigi mabawa au kufungua midomo kwa kupiga kelele. Lakini Yawe anasema hivi:


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Mimi, Yawe, ni mulimaji wake; ninalimwangilia maji kila wakati. Ninalilinda usiku na muchana, kusudi lisiharibiwe na mutu yeyote.


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


Nitakuokoa wewe pamoja na muji huu toka katika mikono ya mufalme wa Asuria na kuulinda.


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.


Alikuwa kama tai anayelinda chicha yake, anayeruka karibu ya vitoto vyake, akitandaza mabawa yake kwa kuwashikilia, na kuwabeba juu ya mabawa yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ