Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 31:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu; farasi wao nao ni nyama tu, si roho. Yawe akiunyoosha mukono wake, taifa linalotoa musaada litajikwaa, na lile linalosaidiwa litaanguka; yote mawili yataangamia pamoja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 31:3
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye ana nguvu za kibinadamu tu, lakini sisi tuna Yawe, Mungu wetu, kwa kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Maneno haya ya mufalme Hezekia yakawatia moyo sana watu wale.


Afazali kumukimbilia Yawe kuliko kumutumainia mwanadamu.


Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi; nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mutu.


Ee Yawe, simama sasa mwanadamu asishinde! Uyakusanye sasa hivi mataifa mbele yako, uyahukumu.


Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?


Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!


Wakati huo, wakaaji wa kandokando watasema: Muangalie yaliyowapata watu tuliowategemea na kuwakimbilia kuomba musaada watuokoe na mufalme wa Asuria! Na sasa, sisi tutaweza namna gani kupona?


Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.


wote watapata haya. Wamisri hawawezi kuwasaidia ninyi, hawawezi kuwapa musaada au faida, lakini watawapatisha haya tu na kuwafezehesha.


Maana musaada wa Misri ni bure, haufai kitu; kwa hiyo nimeipanga Misri jina: Nyoka mukubwa asiyekuwa na nguvu!


Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono yeyote atakayeuegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea.


Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


Ninyi mumenikataa mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ninyi mumeniacha na kurudi nyuma. Kwa hiyo nimenyoosha mukono kwa kuwaangamiza. Nimechoka na kuwahurumia.


Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!


Wapiga upinde katika vita hawataweza kusimama na nguvu; wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kujiokoa, wala waaskari wapanda-farasi hawatayaokoa maisha yao.


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ