Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 31:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 31:1
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu wakamuletea Yosefu nyama wao: farasi, ngombe, kondoo, mbuzi na punda, naye akawapa chakula. Mwaka ule Yosefu akakuwa anawapa chakula kwa kubadilishana na nyama wao wote.


Kwa wakati ule, nabii Hanani akamwendea mufalme Asa wa Yuda, akamwambia: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Suria kuliko kumutegemea Yawe, Mungu wako, jeshi la mufalme wa Suria limekuponyoka.


Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”


Utamutegemea kwa sababu ana nguvu nyingi na kumwacha akufanyie kazi zako nzito?


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Mungu anayekuwa mwangaza wa Israeli atakuwa kama moto. Mutakatifu wa Israeli atakuwa ulimi wa moto ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu, miiba yake na michongoma zake pamoja.


Inchi yao imejaa feza na zahabu, akiba yao ni kubwa zaidi. Inchi yao imejaa farasi, magari yao ya vita hayana hesabu.


Kisha wote waliotegemea Kushi na kujivunia Misri watajuta na kufazaika.


Katikati ya kuta hizo mulijijengea birika la kulinda maji yanapotiririka kutoka birika la zamani. Lakini hamukumutafuta Mungu aliyepanga mambo haya yote; hamukumujali yeye aliyepanga hayo yote tangu zamani.


Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.


Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono yeyote atakayeuegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea.


Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.


Mimi ni Yawe, Mutakatifu wenu; Mimi ndiye Muumba wa Israeli, Mufalme wenu.


Katika karamu zao, hapakosekani vinubi, zeze, ngoma, filimbi na divai. Lakini hawajali matendo ya Yawe, wala kutambua kazi za mikono yake.


Munajipakaa marasi na mafuta kwa wingi kisha munakwenda kumwabudu Moleki. Munawatuma wajumbe wenu huko na huko, kujitafutia miungu ya kuabudu; hata kuzimu walifika.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.


Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.


Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Utamwambia mufalme wa Yuda hivi ambaye amekutuma uniombe kwa ajili yake: Waaskari wa Mufalme wa Misri waliokuja kukusaidia, wako karibu kurudia kwao Misri.


na kusema kwamba mutakwenda kukaa katika inchi ya Misri, ambako hamutaona vita wala kusikia sauti ya baragumu wala kukosa chakula,


Lakini yule mufalme mupya alimwasi mufalme wa Babeli kwa kuwatuma wajumbe Misri kuomba farasi na waaskari wengi. Mufalme huyo atashinda? Anayefanya hivyo na kuvunja agano lake ataweza kuepuka azabu?


Misri haitakuwa tena na nguvu za kuweza kutegemewa na Waisraeli. Waisraeli watakumbuka jinsi walivyokosa kwa kutegemea inchi ya Misri. Waisraeli watatambua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Basi, watarudi katika inchi ya Misri; watatawaliwa na mufalme wa Asuria, kwa sababu wamekataa kunirudilia.


Nitaizuia hasira yangu kali; sitamwangamiza tena Efuraimu, maana mimi ni Mungu, wala si mwanadamu. Mimi ndimi Mutakatifu kati yenu, nami sitakuja kuwaangamiza.


Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.


Wote wamewaka hasira kama furu, na wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wao wote wameanguka, wala hakuna anayeniomba musaada.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Mungu amekuja kutoka jimbo la Temani, Mungu mutakatifu anakuja kutoka mulima Parani. Utukufu wake umeenea pote mbinguni, nayo dunia imejaa sifa zake.


Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.


Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ