Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mungu aliniambia: Sasa andika jambo hili mbele yao, juu ya kibao na katika kitabu, likuwe ushuhuda wa milele:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:8
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Musome katika kitabu cha Yawe: Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana, kila kimoja kitakuwa na mwenzake. Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo. Roho yake itawakusanya hao wote.


Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambapo mutaelewa vema mambo hayo.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Andika katika kitabu maneno yote ninayokuambia.


Twaa kizingo cha kitabu uandike humo maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, juu ya Yuda na mataifa yote, tangu siku nilipoanza kusema nawe, wakati Yosia alipokuwa mufalme mpaka leo.


Halafu Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria. Naye Baruku akaandika katika kitabu maneno yote yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia sawa vile Yawe alivyokuwa amemwambia.


Lakini katika siku zinazokuja nitawarudisha tena Moabu katika hali yao. –Ni ujumbe wa Yawe. Hii ndiyo hukumu juu ya Moabu.


Nilikuwa nimeandika katika kitabu hasara yote niliyotangaza juu ya Babeli na vilevile maneno mengine juu ya Babeli.


Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Kisha, Yawe akanijibu hivi: Uyaandike maono haya; uyaandike wazi juu ya vibao, anayepitia pale apate kuyasoma haraka.


Sasa ninarudi kwa watu wangu, lakini mbele sijaondoka, acha nikuambie mambo ambayo watu hao watawatendea watu wako siku zinazokuja.


“Sasa, andika wimbo huu, uwafundishe watu wa Israeli kusudi ukuwe ushuhuda wangu juu yao.


Basi, Musa akaandika wimbo huo siku hiyohiyo, akawafundisha Waisraeli.


Maana ninajua kwamba nyuma ya kifo changu hakika mutakuwa waovu na kuacha ile njia niliyowaamuru muifuate. Na katika siku zinazokuja mutapatwa na hasara kwa sababu mutafanya maovu mbele ya Yawe na kumukasirikisha kwa matendo yenu.”


Mambo haya yote yatakapowapata huko, kisha mukipata taabu, mutamurudilia Yawe na kumutii.


Roho Mutakatifu anasema wazi kwamba katika nyakati za mwisho, watu wengine watapotoka katika imani yao na kufuata roho za udanganyifu na mafundisho ya pepo.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Wao waliwaambia: “Katika siku za mwisho, kutakuja watu watakaowachekelea, wakiishi kwa kufuata tamaa zao mbaya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ