Wakati huo, wakaaji wa kandokando watasema: Muangalie yaliyowapata watu tuliowategemea na kuwakimbilia kuomba musaada watuokoe na mufalme wa Asuria! Na sasa, sisi tutaweza namna gani kupona?
Yeye alikuwa amewaahidia ninyi: Nitawaonyesha ninyi pumziko, nitawapa pumziko enyi muliochoka. Hapa ni pahali pa pumziko. Lakini wao hawakutaka kunisikiliza.
Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.
Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.
Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?
Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Utamwambia mufalme wa Yuda hivi ambaye amekutuma uniombe kwa ajili yake: Waaskari wa Mufalme wa Misri waliokuja kukusaidia, wako karibu kurudia kwao Misri.
Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.