Yeye ana nguvu za kibinadamu tu, lakini sisi tuna Yawe, Mungu wetu, kwa kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Maneno haya ya mufalme Hezekia yakawatia moyo sana watu wale.
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.
Yawe wa majeshi atainua fimbo yake kama vile alivyowapiga Wamidiani kwenye jiwe la Orebu. Atanyoosha fimbo yake juu ya bahari kama vile alivyowafanyia Wamisri.
Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu.
Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.
Lakini ninyi watu wa Yerusalema mutaimba kwa furaha kama munavyofanya wakati wa makesha ya sikukuu. Mutajaa furaha kama watu wanaotembea kwa mudundo wa muziki wa filimbi kwenda kwenye mulima kwa Yawe, kikingio cha Israeli.
Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.
Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu. Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali, akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili, sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi. Ulikuwa na mapambo ya zahabu. Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.
Nitayashitusha mataifa mengi kwa habari zako, wafalme wao watatetemeka kwa sababu yako, nitakaponyoosha upanga wangu mbele yao. Watatetemeka kila wakati, kila mutu akiogopea maisha yake, siku ile ya kuangamia kwako.
Katika wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ametuahidi hivi: “Nitatetemesha dunia mara moja tena, wala si dunia tu, lakini mbingu vilevile.”
Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.
Waaskari walipokuwa wanarudi kwenye nyumba, pamoja na Daudi kisha kumwua yule Mufilistini, wanawake kutoka kila muji katika Israeli walitoka kwenda kumupokea mufalme Saulo. Wanawake nao walikuwa wanaimba nyimbo za furaha, wakipiga matari na vinubi.