Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:23
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

nikaona ngombe saba wazuri na wanono wakitoka katika muto na kula nyasi.


Ngombe wale saba wazuri ni miaka saba, na yale masuke saba mazuri vilevile ni miaka saba. Ndoto hiyo tafsiri yake ni moja.


Katika miaka ile saba ya shibe, mashamba ya Misri yakatoa mazao kwa wingi sana.


Kweli wema wako ni bora! Wanadamu wanakimbilia kwenye kivuli cha mabawa yako.


Inchi imetoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, ametubariki.


Wakati huo, muzigo waliowabebesha atauondoa na nira waliyowatia kwenye shingo lenu itavunjwa. Adui amepanda kutoka Rimoni,


Lakini heri yenu ninyi: mutapanda mbegu zenu popote penye maji, ngombe na punda wenu watatembeatembea namna wanavyotaka.


Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.


Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Mimi Yawe nitawaongoza siku zote, nitatimiza mahitaji yenu wakati wa shida. Nitawaimarisha katika mwili, nanyi mutakuwa kama bustani iliyomwangiliwa maji, kama chemichemi ya maji ambayo maji yake hayakauki hata kidogo.


Watu watajenga nyumba na kuishi humo; watalima mizabibu na kula matunda yake.


Katikati ya miungu ya uongo ya mataifa nani anayeweza kunyesha mvua? Au, ni mbingu ndiyo inaweza kutoa manyunyu? Si ni wewe ee Yawe, Mungu wetu? Tunakuwekea wewe tumaini letu, maana ni wewe unayefanya haya yote.


Waisraeli ni wenye kichwa kigumu kama punda. Kwa nini basi Mungu ashugulike na kuwachunga, kama kondoo katika shamba kubwa la kuwakulishia?


Inchi itatoa mazao yake nanyi mutakula na kushiba na kuishi mule kwa usalama.


Kama mukifuata masharti yangu na kushika amri zangu,


Kupepeta ngano kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na mavuno ya zabibu mpaka wakati wa kupanda mbegu. Mutakuwa na chakula tele na kuishi kwa usalama katika inchi yenu.


Muombe Yawe awape mvua za masika. Yawe ndiye anayeleta mawingu ya mvua; ndiye anayewapa watu mvua za manyunyu, na kustawisha mimea katika shamba kwa ajili ya wote.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


yeye ataipatia inchi yenu mvua wakati wake, mvua za kwanza na mvua za mwisho, nanyi mutavuna ngano yenu, divai yenu na mafuta yenu.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ