Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:19
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.


Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.


Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Siku ya kuwakomboa inakaribia, haiko mbali tena; siku ya kuwaokoa ninyi haitachelewa. Nitauokoa Sayuni, nitaleta utukufu kwa Israeli.


Halafu mutaomba, nami Yawe nitawaitikia; mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada, nami nitajibu hivi: Niko hapa! Kama mukiondoa mambo ya kitumwa, mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,


Mwangaza wako muchana hautatua kama jua, wala mwangaza wako usiku kufifia kama mbalamwezi; maana Yawe ni mwangaza wako milele, nazo siku zako za kuomboleza zitakoma.


Mufurahi na kushangilia milele, kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba. Yerusalema nitaifanya muji wa shangwe, na watu wake watu wenye furaha.


Nami nitaufurahia Yerusalema, nitawafurahia watu wangu. Sauti ya kilio haitasikilika tena, kilio cha taabu hakitakuwa tena.


Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


Nitawajalia watu wa Yakobo, na Yuda nitamujalia watakaorizi milima yangu; wachaguliwa wangu watairizi, watumishi wangu watakaa kule.


Yawe anasema hivi: Mapigo yako hayaponi, vidonda vyako haviwezi kutunzwa.


Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.


Yawe anasema hivi: Acha kulia, panguza machozi yako, maana utapata malipo kwa kazi yako. –Ni ujumbe wa Yawe.– Watoto wenu watarudi kutoka inchi ya waadui zenu.


Maana kutakuja siku ambapo walinzi watalalamika hivi katika vilima vya Efuraimu: Musimame, tupande kwenda Sayuni kwa Yawe, Mungu wetu.


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.


Yawe amehakikisha kwamba hatuna kosa. Tuende Sayuni tutangaze matendo ya Yawe, Mungu wetu.


Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule. –Ni ujumbe wa Yawe.– Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waisraeli wataniomba niwafanye kuwa wengi kama kundi la kondoo, nami nitawafanya hivyo.


Sasa kwa nini munalia kwa sauti? Hamuna mufalme tena? Mushauri wenu ametoweka? Munalalamika kwa uchungu, kama mwanamuke anayezaa!


Heri kwenu munaokuwa wenye njaa sasa, maana mutashibishwa. Heri kwenu munaolia sasa, maana mutacheka.


Na halafu taifa lote la Israeli litaokolewa kama vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mukombozi atatokea Sayuni, atakomesha uovu kati ya wazao wa Yakobo.


Basi, Mungu ambaye kwa nguvu yake inayofanya kazi ndani yetu, anaweza kufanya mambo makubwa zaidi yanayopita yale tunayoweza kuomba au kufikiri;


Nami nikalia sana, kwa sababu hakukuonekana mutu aliyestahili kufungua kizingo wala kuangalia ndani yake.


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ