Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:18
69 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atakujibu namna gani wakati wewe unasema kwamba haumwoni na kwamba maneno yako iko mbele yake na wewe unamungojea!


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu, na kuwaokoa kutoka katika hatari.


Yawe Mungu ni jua na ngao yetu. Anatukubali na anatupatia utukufu. Hawanyimi kitu chochote kizuri wale wanaoishi katika ukamilifu.


Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.


Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena: Yawe, Yawe, ni Mungu mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa wema na uaminifu.


Anayefikiri sana juu ya neno atafanikiwa. Heri mutu yule anayemutumainia Yawe.


Maana, Yawe ameniambia hivi: Tokea juu kwenye makao yangu nitaangalia yanayotukia, nikitulia kama joto katika mwangaza wa jua, kama wingu la umande wakati wa mavuno.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.


Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.


Yawe ametukuzwa, yeye anaishi juu mbinguni. Ameujaza Sayuni usawa na haki.


Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.


Yawe anasema hivi: Kwa muda murefu sasa nimenyamaza, nimekaa kimya na kujizuiza; lakini sasa nitalia kama mwanamuke wakati wa kuzaa, anayeugua pamoja na kupumua kwa nguvu.


Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.


Kwa heshima ya jina langu, ninatuliza hasira yangu; kwa ajili ya heshima yangu, ninajizuiza kusudi nisikuangamize.


Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa wakati sheria yake inafuatwa. Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa wakati haki inatendwa.


Maana mawazo yangu si kama mawazo yenu, wala njia zangu si kama njia zenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Abarikiwe mutu anayenitegemea mimi Yawe, mutu ambaye mimi Yawe ndiye tegemeo lake.


Nyuma ya siku kumi, neno la Yawe lilimufikia Yeremia.


Heri yao watakaovumilia mpaka siku zile elfu moja mia tatu na makumi tatu na tano zitakapotimia.


Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.


Nitaiharibu mizabibu yake na tini zake, anayosema ni malipo kutoka kwa wapenzi wake. Nitaifanya ikuwe pori, nao nyama wa pori wataikula.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Mumemuchokesha Yawe kwa maneno yenu matupu. Hata hivyo, munasema: Tumemuchokesha namna gani? Mumemuchokesha munaposema: Yawe anawaona kuwa wazuri watu wanaotenda mabaya; tena anawapenda. Au munapouliza: Yuko wapi yule Mungu mwenye haki?


Kisha akafunga safari yake na kurudia kwa baba yake. “Alipokuwa angali mbali kidogo, baba yake akamwona, akamusikilia huruma. Akamukimbilia, akamukumbatia mwana wake na kumubusu.


Wakati ule katika Yerusalema kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Simeoni. Mutu huyo alikuwa mwenye haki na mwenye kuogopa Mungu. Alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa taifa la Israeli. Roho Mutakatifu alikuwa pamoja naye;


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Basi kuna nini? Mungu alitaka kuonyesha kasirani yake na kutambulisha uwezo wake. Lakini aliwavumilia sana wale waliostahili kupatwa na kasirani yake na waliokuwa wametayarishwa kwa kuangamizwa.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Tunawaita watu hao kuwa wenye heri, kwa sababu walivumilia. Mumekwisha kusikia habari za uvumilivu wa Yobu, na munajua namna Bwana alivyomutendea kwa mwisho. Maana Bwana anajaa huruma na wema.


Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.


Bwana hakawii kutimiza ahadi zake kama vile watu wamoja wanavyozania. Yeye anavumilia kwa ajili yenu, maana hapendi hata mutu mumoja apotee, lakini anataka watu wote wageuke toka zambi zao.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ