Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui; na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote. Kwa mwisho, watakaobaki, watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima, kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:17
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Hata kama mukiwashinda waaskari wote wa Wakaldea wanaopigana nanyi na kunabaki tu katika mahema yao wale walioumizwa, hao watasimama na kuuteketeza muji huu kwa moto.


Waliotufuatilia walikuwa wepesi kuliko tai, walitukimbiza kwenye milima walituvizia katika jangwa.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


Na kwa njia ya wamoja wenu watakaobaki nitaleta woga ndani ya moyo wao, katika inchi ya waadui zao hata jani linalopeperushwa litawakimbiza. Watakimbia kama mutu anayekimbia vita. Watakimbia na kuanguka hata kama hakuna mutu anayewafukuza.


Watano wenu watafukuza waadui mia moja na mia moja wenu watafukuza waadui elfu kumi. Waadui zenu wataangamia mbele yenu kwa upanga.


Hata wale wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kutoroka; wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na waaskari watashindwa kuyaokoa maisha yao.


Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Matawi mamoja ya muzeituni uliopandwa yamekatwa, na chipukizi la muzeituni uliojiotesha katika pori umepandikizwa kwenye nafasi yao. Na sasa unafaidia vilevile utomvu unaotoka ndani ya shina la yule muzeituni uliopandwa.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?


Mutu wenu mumoja tu anaweza kuwakimbiza waadui elfu moja, maana Yawe Mungu wenu ndiye anayewapigania kama alivyowaahidi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ