Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:16
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini waaskari wa Babeli wakamufuata mufalme na kumuteka kwenye bonde za Yeriko, nao waaskari wake wote wakamwacha, wakatawanyika.


Utamutegemea kwa sababu ana nguvu nyingi na kumwacha akufanyie kazi zako nzito?


Yeye hafurahii nguvu za farasi, wala hapendezwi na ushujaa wa waaskari;


Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi; nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mutu.


Inchi yao imejaa feza na zahabu, akiba yao ni kubwa zaidi. Inchi yao imejaa farasi, magari yao ya vita hayana hesabu.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu; farasi wao nao ni nyama tu, si roho. Yawe akiunyoosha mukono wake, taifa linalotoa musaada litajikwaa, na lile linalosaidiwa litaanguka; yote mawili yataangamia pamoja.


Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani.


Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!


Wanaokuwa wepesi hawawezi kutoroka, mashujaa hawawezi kukwepa; huko kaskazini kwenye muto Furati wamejikwaa na kuanguka.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa na waaskari walikimbia. Wakatoka inje ya muji wakati wa usiku wakipitia njia ya mulango katikati ya kuta mbili, kwenye bustani ya mufalme, ingawa Wakaldea walikuwa wameuzunguka muji wote. Wakakimbia kuelekea bonde la muto Yordani.


Waliotufuatilia walikuwa wepesi kuliko tai, walitukimbiza kwenye milima walituvizia katika jangwa.


Nilimwona Yawe akisimama pembeni ya mazabahu, naye akaniamuru: Piga zile nguzo za hekalu mpaka misingi yake itikisike. Uvunje zile nguzo ziwaangukie watu juu ya vichwa. Wale watakaobaki nitawaua kwa upanga; hakuna hata mumoja wao atakayeponyoka, hakuna atakayetoroka.


Enyi wakaaji wa Lakisi, mufunge farasi wepesi na magari ya vita. Ninyi mulikuwa mumeiga zambi ya watu wa Sayuni, makosa ya Waisraeli yalikuwa kwenu.


Farasi wao ni wepesi kuliko chui, wakali kuliko imbwa wa pori wenye njaa. Waaskari wapanda-farasi wao wanatoka mbali, wanaruka mbio kama tai anavyorukia nyama.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


“Yawe ataleta kutoka mbali taifa moja liwashambulie mbio kama tai, taifa ambalo hamujui luga yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ