Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kuporomoka kwa ukuta huo, ni kama kupasuka kwa chungu ambacho kimepasuliwa vibaya sana, bila kubaki kigae cha kuopolea moto ndani ya jiko, au kuchotea maji katika kisima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:14
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Upepo ule unamufunika bila huruma; anajaribu kukimbia lakini mbio za bure.


Utawaponda kwa fimbo ya chuma, utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ”


Waadui zangu wote wananizarau, na hasa zaidi wenzangu. Warafiki zangu wameniona kuwa kitisho; wanaponiona katika njia wananikimbia.


Kutokana na hayo hasara itamupata kwa rafla; kwa rafla atapondekana vibaya wala hatapata kupona.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Wao ni kama majani yenye kukauka: moto utayateketeza! Hawawezi hata kujiokoa wenyewe mbali na ukali wa moto huo. Moto huo si wa kujipatia joto, huo si moto wa kuota!


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Nitawagonganisha wao kwa wao hata baba na watoto. –Ni ujumbe wa Yawe.– Sitawahurumia, sitawaachilia wala sitawarehemu, mpaka nitakapowaangamiza.


Juu ya nyumba za Moabu na katika viwanja vyao hakuna kinachosikilika lakini maombolezo tu. Mimi nimemuvunja Moabu kama chombo kisichotakiwa na mutu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Watoto wa Sayuni waliosifiwa sana, waliokuwa na bei kama zahabu safi, namna gani sasa wamekuwa kama vyombo vya udongo, kazi ya mikono ya mufinyanzi!


Ni mimi Yawe ninayesema hivyo. Jambo hilo litakamilika; mimi nitalitenda. Sitajuta jambo hilo wala kukuonea huruma. Nitakuazibu kulingana na mwenendo na matendo yako. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– kwa vile mumechafua Pahali Patakatifu pangu, kwa matendo yenu mabaya na machukizo yenu, mimi nitawaangamiza bila huruma na bila kumwacha mutu yeyote.


Sitawaachilia wala sitawaonea huruma. Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu, nayo machukizo yenu yangali bado kati yenu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Sitawaachilia wala sitawaonea huruma. Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu nayo machukizo yangali bado kati yenu. Halafu mutatambua kwamba ni mimi Yawe ninayewaangamiza.


Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.


Kwa upande wangu, sitawaachilia wala kuwahurumia; nitawatendea kufuatana na matendo yao.


Kule akajaribiwa na Shetani kwa muda wa siku makumi ine. Kwa muda ule, yeye hakukula kitu. Na wakati siku zile zilipotimia, akasikia njaa.


Kwa maana ikiwa Mungu hakuachilia yale matawi ya asili kuendelea kukomaa, namna gani atakuachilia wewe?


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.


Atayatawala kwa fimbo ya chuma na kuyaponda kama vile mutungi,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ