Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 30:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Basi, zambi hii itakuwa kwenu kama ufa mukubwa katika ukuta murefu; utabomoka mara moja na kuanguka chini kwa rafla.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 30:13
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waliobaki, walikimbilia katika muji wa Afeki. Kule, kuta za muji ziliwaangukia na kuwaua watu elfu makumi mbili na saba waliobakia. Beni-Hadadi vilevile alikimbia na kujificha katika chumba fulani cha ndani, katika muji.


Angalia kasirani isikuvute kwa kuzarau, au usiache ukubwa wa mali za kukukomboa ukupotoshe.


Yeye peke yake ndiye kikingio na wokovu wangu, yeye ni kimbilio langu, sitatikisika.


Mpaka wakati gani mutanishambulia mimi? Mpaka wakati gani ninyi wote mutanipiga, mimi ninayekuwa kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Kutokana na hayo hasara itamupata kwa rafla; kwa rafla atapondekana vibaya wala hatapata kupona.


Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema: Hakika uovu huu hautasahauliwa mbele ya kufa kwenu. Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.


Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Lakini hasara itakupata ambayo hautaweza kujiepusha nayo. Magumu yatakutokea ambayo hautaweza kuyapinga; maangamizi yatakufikia kwa rafla ambayo haujapata kuyaona hata kidogo.


Nilitangaza zamani matukio ya mbele, niliyatangaza mimi mwenyewe na kuyafanya yajulikane kwenu. Mara moja nikaanza kuyatimiza, nayo yakapata kutukia.


Watu wako watajenga tena mabomoko ya zamani; mutajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani. Nanyi mutaitwa watu waliotengeneza upya kuta, watu waliotengeneza tena barabara za miji.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Mvua ikanyesha, mito ikajaa, upepo ukavuma na kupiga nyumba ile, nayo ikaanguka na kubomoka kabisa.”


Lakini yule anayesikia maneno yangu pasipo kuyashika, anafananishwa na mutu aliyejenga nyumba juu ya udongo bila kuchimba musingi. Maji kutoka muto yakaishambulia, na mara moja ikaanguka na kubomoka kabisa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ