Wakati uleule, Wafilistini walikuwa wakiishambulia miji ya Sefela na Negebu ya Yuda. Walinyanganya miji ya Beti-Semesi, Ayaloni, Gederoti, Soko na vijiji vyake, Timuna na vijiji vyake, Gimuzo na vijiji vyake, wakafanya makao yao kule.
Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.
Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.
Lakini jambo la “Muzigo wa Yawe”, musilitaje tena. Neno mwanadamu analosema litakuwa muzigo kwake mwenyewe, kwa maana munageuza maneno yangu mimi Mungu Mwenye Uzima, Yawe wa majeshi, Mungu wenu.
Katika siku Hezekia alipokuwa mufalme wa Yuda, Mika wa Moreseti aliwatangazia watu wote kwamba Yawe wa majeshi alisema hivi: Sayuni utalimiwa kama shamba, Yerusalema utabaki mabomoko, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.
basi, nitaiharibu nyumba hii kama nilivyoharibu ile ya Shilo, na nitaufanya muji huu kuwa mufano kwa mataifa yote ya dunia yatakaoutumia kwa kutoa laana.
Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!
Imekuwa hivyo kwa sababu ya uovu walioufanya, wakanikasirikisha kwa kuifukizia ubani na kuitumikia miungu mingine ambayo wao wenyewe hawakuifahamu, wala ninyi, wala babu zenu.
Uchafu wake ulionekana waziwazi, lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake. Anguko lake lilikuwa kubwa sana; hakuna anayeweza kuufariji. Unasema: Angalia, ee Yawe, mateso yangu, maana adui yangu ameshinda.
Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeona mambo wazee wa Waisraeli wanayotenda kwa uficho, kila mutu katika chumba chake cha sanamu. Wanasema: Yawe hatuoni. Yawe ameiacha inchi.
Naye akaniambia: Uovu wa Waisraeli na watu wa Yuda ni mukubwa sana. Inchi imejaa umwagaji wa damu na katika muji hakuna haki, kwa maana wanasema: Yawe ameiachilia inchi; Yawe haoni.
Wanaigeukia miungu ya bure, wako kama upinde ulioregea. Waongozi wao watakufa kwa upanga, kwa sababu ya maneno yao ya kiburi. Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.
Wewe ni mutakatifu kabisa, hauwezi kutazama uovu, hauwezi kuvumilia hata kidogo kuona mabaya. Mbona basi unawaona wafanya maovu na kunyamaza, kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao?
Atakuja kuwahukumu wote na kuwaazibu watu wabaya wasiomwogopa Mungu, kwa ajili ya matendo yao yote mabaya waliyotenda, na kwa ajili ya maneno yote mabaya wenye zambi hawa waliyosema juu yake.”